Posts

KUPINGWA KIPANDE CHA KICHAWI

 Uchawi kipande Nini? Imeitwa uchawi wa KIPANDE kwa kuwa kinachotumika ni uchawi uliowekwa kwenye KIPANDE CHA mti ambacho baada ya juunganishwa hurushwa na kuondoka mpaka kwa aliyekusudiwa na kupenya ndani ya mwili na kumuathiri.  Mchawi hutafuta mzizi wowote unaofuata njia, Kisha hukata KIPANDE chenya urefu nchi 4 au 5 kisha hutoboa na kuweka vifaa kama samaki anayepiga shoti (kunta) kisiki cha njiani, samaki munzolo, vumbi la mti uliopigwa na radi, kinyonga aliyejifia, chura aliyegongwa na gali. K

JINI WA KUTUMWA

 Tulisema upo uchawi wa kila aina, na tulizungunzia uchawi wa kifungo na faraka kutoka bara na pwani. Sayansi ya kichawi imefanikiwa kutengenezea mapepo na kumtumia mtu, Pepo hilo linaweza kupanda katika kichwa cha aliyelogwa na kuzungumza, na hutumwa kwa nia mbalimbali, mchawi anaweza kutengenezea pepo akaliingiza katika mwili wako ili kufunga kazi zako au kukuletea kila aina ya magonjwa ikiwepo kiharusi. Pepo ambalo pia huitwa jini wa kutumwa, hutengenezwaje? Kwanza mchawi hutafuta udongo wa kisuguu cheusi, ambacho nchwa wanapandisha udongo mbichi. Udongo huo huchanganywa na mchanga kidogo wa kaburi tatu na mchanga wa njia mbili zinazo pishana (njiapanda) Kisha hutengeneza sanamu linalo lingana na jinsia ya mtu anayetaka kumloga. Mchawi hutoboa juu ya kichwa cha sanamu Kisha huweka vifaa vya mtu anaye mkusudia, vifaa hivyo ni kati ya nywele, nyuzi za nguo yake, nyayo na kadhalika akikosa hivyo hutumia jina lake tu.  Kisha hutoboa tumbo na kuweka funza saba wanaotokana na dam...

UCHAWI WA PWANI

 Tuliona katika Afrika uchawi umegawanyika katika sehemu ya bara na pwani, kwa ufupi tulitaja uchawi wa bara tukaonyesha watu wa eneo hilo namna wanavyo tengeneza uchawi wa kifungo na faraka, swali ambalo watu wengi wanauliza, watu wa pwani wanatengenezaje uchawi wa kifungo na faraka? Kwanza nikiri wazi kuwa pwani kuna uchawi tofauti na bara kwa kuwa katika eneo hilo walipitia wageni kutoka nga'mbo kwa majahazi na meli, baadhi yao waliweka makazi yao katika eneo hilo. Baadhi ya wageni hao ni pamoja na Wareno, Waitali, Waingereza, Wafaransa na Waarabu. Unakumbuka katika Babeli Iraq ya sasa, alikuwepo mchawi mkubwa aliyeitwa Nimrod aliyezaliwa mwaka 2200- l2154 kabla ya Yesu, bwana huyo alikuwa mfalme aliyeishi wakati wa nabii Ibrahimu, baadaye akajiita Mungu na kuwataka watu wamuabudu. Aidha unakumbuka katika eneo jirani waliishi Waajemi eneo ambalo kwa sasa inapatikana nchi ya Iran? Watu wa eneo hilo walikuwa wachawi hatari. Katika eneo la Afrika nchini Misri alikuwepo mfalme aliye...

UCHAWI TATIZO LA DUNIA

 Katika makala iliyotangulia tulijikumbusha kwamba Mwenyezi Mungu aliumba mitishamba kwa lengo la kumnufaisha mwanaadamu. Kwa hekima zake alimuumba mwanaadamu kutokana na udongo, ndani ya udongo huo akaweka kila aina ya madini yanayo hitajika katika mwili wa mwanaadamu ili kuujenga na kuulinda. Kadhalika tuliona uchawi ambao ni zao la shetani ulivyopata wafuasi dunia nzima na kuiathiri jamii ya mwanaadamu. Katika sehemu hii tutaangalia kwa ufupi aina mbili za uchawi na unavyoandaliwa. Kuna uchawi wa kila aina kulingana na eneo, kwa mfano katika nchi za Afrika uchawi umegawanyika katika sehemu kuu mbili, uchawi wa bara na uchawi wa pwani. Uchawi wa pwani ni tofauti na uchawi wa bara kwa sababu watu wa pwani walipata wageni wengi kutoka sehemu mbalimbali za dunia, hasa Wazungu na Waarabu baadhi ya wageni waliwafundisha wenyeji uchawi mpya kabla na wao kujifundisha uchawi wa wenyeji. Kabla hatujaona kwa muhtasari namna uchawi unavyoandaliwa, ni muhimu kuzingatia lengo la makala haya, ...

Hekima ya Mungu kuumba miti

 Mwenyezi Mungu alimuumba mwanaadamu kutokana na udongo, ndani ya udongo akaweka kila kitu kinachohitajika katika mwili wa mwanaadamu kama madini na vitamani za kila aina. Ili mwanaadamu aweze kuishi salama katika dunia, ili kuwa ni muhimu aendelee kuyatumia madini na bidhaa kadhaa alizoumbiwa, ambazo zinapatikana kwa wingi ardhini. Mwenyezi Mungu kwa hekima kubwa akaotesha miti na majani yanayo fyonza madini na virutubisho kutoka katika udongo. Mpaka hapo utaona kuna umuhimu kiasi gani kutumia bidhaa za mitishamba katika kuutibu mwili wa mwanaadamu katika kuurudishia mali ghafi za asili alizoumbwa nazo.  Katika makala zetu hizi tutajaribu kutafakari pamoja uzowefu wetu katika siri kubwa aliyoiweka Muumba wetu ndani ya miti pamoja na majani. Kadhalika tutaangalia namna ya kujitibu maradhi yanayotokana na nguvu za giza. Ni ukweli ukiowazi kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kumuumba mwanaadamu shetani wa kijini aliumizwa mno kutokana na karama alizotunukiwa mwanaadamu, hivyo aliapa ku...